Saturday, February 28, 2015

JUMAMOSI YA NENO

Neno la leo limetoka katika kitabu cha Nabii Yeremia 33:1-6
1 Tena, neno la Bwana likamjia Yeremia mara ya pili, hapo alipokuwa akali amefungwa katika uwanda wa walinzi, kusema,
2  Bwana alitendaye jambo hili, Bwana aliumbaye ili alithibitishe; Bwana ndilo jina lake; asema hivi,
3  Niite, nami nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua.
4  Maana Bwana, Mungu wa Israeli asema hivi, katika habari za nyumba za mji huu, na katika habari za nyumba za wafalme wa Yuda, zilizobomolewa ili kuyapinga maboma na upanga;
5  Wanakuja kupigana na Wakaldayo, lakini ni kuzijaza kwa mizoga ya watu, niliowaua katika hasira yangu na ghadhabu yangu, ambao kwa ajili ya uovu wao wote nimeuficha mji huu uso wangu.
6  Tazama, nitauletea afya na kupona, nami nitawaponya; nami nitawafunulia wingi wa amani na kweli. 

Waliotungozea neno la leo ni Mwlm Peter Mzuli, Innocent Mosha na Marystella Leonard



Thursday, February 26, 2015

MUNGU ASANTE

Tuna kila sababu ya kusema Mungu asante kwa kila hatua tunayoipitia, tunaamini kuwa kupitia maombezi ya Mtakatifu Lucia, tutasimama imara katika kumteteaYesu  Kristu aliye njia ya kweli na uzima. Na pia kulitangaza neno la Mungu kwa njia ya uimbaji. Tunaziombea kwaya  zote ziweze kuinjilisha katika Roho na Kweli. Amina
 
Haya ni mahudhurio ya kawaida kwa sauti ya kwanza

 Hawa ni baadhi ya sauti ya Pili

Hawa ni baadhi ya Sauti ya Tatu

Na hawa ndio baadhi ya wababa wa kwaya(yaani sauti ya nne)

Saturday, February 21, 2015

JUMAMOSI YA NENO

Neno la leo limetoka Waraka wa 2 wa mtume Paulo kwa Wakoritho, sura ya 4, aya ya 1-6